Monday, December 26, 2016

ZAMA ZA GIZA;S/N17



         I.            MAFUNGU MATATU YANAYOFANANA MAANA ZAKE

§  Naye atanena maneno  kinyume chake aliye juu ,naye atawadhoofisha  watakatifu wake aliye juu  naye  ataazimu  kubadili majira na  sheria   nao  watatiwa mikononi mwake  KWA WAKATI  NA NYAKATI MBILI NA NUSU  WAKATI. DANIELI: 7:25,

§  Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambapo ana mahali palipotengenezwa na Mungu, ili wamlishe huko MUDA WA SIKU ELFU NA MIA MBILI NA SITINI    UFUNUO: 12:6,

§  Naye akapewa kinywa cha kunena maneno makuu, ya makufuru. Akapewa uwezo wa kufanya kazi yake MIEZI AROBAINI NA MIWILI   UFUNUO 13:5

 

     II.            KUMBUKA SIKU MOJA KIUNABII HUWAKILISHA MWAKA MMOJA EZEKIELI 4:6

 

III.            MAFUNGU MATATU DANIELI 7:25, UFUNUO 12:6,NA UFUNUO 13:5 haya yote yana maana moja –huwakilisha siku 1260  sawa na miaka halisi 1260 jifunze kama ifuatavyo

·         KWA WAKATI –Huwakilisha mwaka mmoja ambao una siku 360 ,NYAKATI MBILI –Huwakilisha miaka miwili ambao  ni sawa na siku 720,NUSU WAKATI-Huwakilisha nusu mwaka ni sawa na siku 180 .Ukijumlisha siku hizo utapata siku 1260 (Danieli 7:25)

·        MUDA WA ELFU MBILI na mia mbili na sitini ni sawa na siku halisi 1260 (ufunuo 12:6)

·        MIEZI AROBAINI NA MIWILI –Ni sawa na siku 1260(yaani 42 mara 30) kumbuka mwezi halisi wa Mungu unasiku 30 tu (ufunuo 13:5)

 

  IV.            MAJINA YA MAKUFURU - Ni maneno ya kumtukana Mungu, dini, unajisi,ukufuru,tamko au maneno ya ambayo  ni kinyume na imani ya dini,dharau ya dini na pia tendo la kudai  sifa  au mamlaka  ya Uungu

 

     V.            HISTORIA FUPI YA ZAMA ZA GIZA

PEMBE NDOGO ATAWADHOOFISHA WATAKATIFU WAKE ALIYE JUU

Wakati wa zama za giza .ambao ulianza katika mwaka wa 538 BK (A.D) wakristo wapatao millioni 50,000.000 KANISA  LA KIRUMI NA MADHEHEBU yake liliwatesa mpaka kufa .habari hii ya kuogofya  ni  historia moja ya giza  kabisa  katika  historia ya mwanadamu .sasa tutumie maneno ya waandishi furani wa historia

Kwamba kanisa la Rumi limemwaga sana damu isiyo na hatia  kuliko wakati wo wote  ulioanzishwa uliokuwako zamani kati ya wanadamu ,kwa mprostanti aliye na mjuzi wa historia  hatakuwa  na shaka.soma kitabu cha LECKS “HISTORIA OF RATIONALISM IN EUROPE.VOL,11,P.32

Mwanandishi  wa kanisa la kirumi anasema  hakika kanisa la kirumi limetesa…….miaka mia  na hamsini baada ya Constantine wakrisro  wa  waafrika kaskazini (donatists) waliteswa katika  ufararansa na Spain kwa kibali kamili  cha kanisa soma “THE WESTERN WATCHMAN DEC.24,1908

PAPA MARTINI v (A.D.1417-1431A.D) alitoa  mafundisho haya  yafuatayo kwa  mfalme  wa Poland kwa  sababu ya  wafuasi wa john huss ambao walikuwa wakristo wa kweli ifanye kazi ya kuwakomesha  wahusiti(“hussites)….geuza uso wako  juu ya wabohemia ,teketeza ,chinja ovyo ovyo wanaume na wanawake na watoto fanya mahame kila mahali…soma L.M.DE CORNAMENIN,THE PUBLIC AND PRIVATE HISTORY OF POPE OF ROME,VOL 11.PP.116,117

VI.            ZAMA ZA GIZA ZILIANZA LINI?

JE UPAPA ULIENDELEA KWA MUDA GANI KATIKA MAMLAKA KUU KATIKA ULAYA?

Mfalme  JUSTINIA wa ROMA  alitoa amri  ya kuwa ASKOFU WA ROMA  PAPA awe ndiye  MKUU WA MAKANISA yote .Amri hii  ilianza kutuimika  A.D 538 wakati WA –ANIANI WA OSTROGOTHS  walipofukuzwa kutoka ROMA . walipofukuzwa  kutoka Roma .katika  mwaka huo  madaraka  ya kidunia  ya upapa  yalianza  ambayo yaliendelea  bila kupungua  katika mapambano  ya miaka  1260 mpaka mwaka wa maangamizi  A.D 1798  ambapo JEMADARI WA UFARANSA BERTHIER ALIPOINGIA ROMA  AKATANGAZA JAMHURU NA KUMTEKA NYARA PAPA

VII.            WITO MUNGU ANAWATIA MOYO WAFUASI WAKE WAAMINIFU KATIKA VIZAZI VYOTE

UFUNUO 12:11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.UFUNUO 2:10 Usiogope mambo yatakayokupata; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima

Mpendwa panga kutokosa somo linalofuata lilasema  kwa nini MAREKANI NIA TAIFA LENYE NGUVU KUBWA DUNIANI .

 

No comments:

Post a Comment