Monday, December 19, 2016

MNYAMA WA TATU NI CHUI-S/N 12



Kisha nikatazama, na kumbe! Mnyama mwingine, kama chui, naye juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege; mnyama huyo alikuwa na vichwa vinne; akapewa mamlaka DANIELI 7:6 , Na baada ya zamani zako utainuka ufalme mwingine mdogo kuliko wewe; na ufalme mwingine wa TATU WA SHABA, utakaoitawala dunia yote DANIELI 2:39

1.      MNYAMA -Huwakilisha ufalme DANIELI 7:17

 
2.    MABAWA MANNE- Yaliwakilisha Mwendo  wa haraka wa kushida kwake

 
3.    VICHWA VINNE -Huwakilisha mgawanyiko wa ufalme katika falme nne mbalimbali baada ya kufa kwake

 
4.    CHUI NA MADINI YA SHABA –Huwakilisha utawala wa WAYUNANI
 

5  UTAWALA huu ulianza kutawala Ulimwengu tangu  mwaka 331 B.C-168 B.C

6.     MFALME aliyetawala utawala huu alikuwa ni  ALEKSANDA MKUU na baada ya kufa kwake makamanda wake  walitawala badala ya yake


7.    IFUATAYO NI HISTORIA FUPI

Ufalme huu ndio wa mapaja ya shaba  ya sanamu  uliokuwa ufalme wa Wayunani uliosimamishwa kwa kushiinda upesi kwa ALEKSANDA MKUU .Chui ni mnyama mdogo  akilinganishwa na Dubu .tunasoma …kama watu 47000 tu walikuwa katika jeshi la ALeksanda  lilishinda jeshi kubwa  sana lenye watu  karibu milioni moja ,MABAWA manne yanaonyesha mwendo  wa haraka  kushida ule wa babeli  juu  ya sehemu  ya jeshi  liloshinda  .Aleksdanda  alikuwa maarufu kwa matengenezo      yake ya hakili  na mwendo wa haraka  vichwa  vinne  huonyesha  mgawanyiko  wa ufalme  wake   katika  falme  nne  mbmbali  baada ya kufa kwake .

8.    Mpendwa usikose somo linalofuata maana linazungumzia manyama wa nne ni mnyama wa kutisha  sana maana hakufanana na mnyama yoyote Mungu akubariki sana unapoendelea kuuchunguza ukweli huu wa biblia.

 

 

No comments:

Post a Comment