Monday, December 26, 2016

YESU ANAPORUDI MARA YA PILI NINI KITATOKEA?;S/N18


YAFUATAYO NI MATUKIO YATAKAYOAMBATANA NA UJIO WA YESU ;
     I.            JE NI KITU GANI YESU ANASUBULI SASA HIVI?
MATHAYO 24:14 Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.kazi hii itakapomalizika Yesu atarudi mara ya pili
II.            JE KUTAKUWA NA ISHARA GANI YA KUMTAMBULISHA YESU ANAPOKUJA?
MATHAYO 24:27 Kwa maana Kama vile UMEME utokavyo mashariki ukaonekana hata magharibi, hivyo ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.
III.            JE NI WINGU GANI LITAONEKANA KAMA UTAMBULISHO WA MFALME WA WAFALME?
Wingu dogo jeusi litaonekana upande wa mashariki.Mfalme   wa wafalme atashuka  na wingu  lililozungushiwa  moto unaowaka .dunia itatetemeka mbele  yake “Mungu  wetu atakuja  wala  hatanyamaza  moto utakula  mbele  zake  na tufani  yavuma sana  ikimzunguka  pande  zote . Ataziita mbingu zilizo juu na nchi pia awahukumu watu wake ZABURI 50:3-4
IV.            JE KUTAKUWA NA MAKUNDI MANGAPI YATAKAYOMUONA YESU ANAPORUDI?
Ufunuo 1:7 Tazama, yuaja na mawingu; na kila jicho litamwona, na hao waliomchoma; na kabila zote za dunia wataomboleza kwa ajili yake. Naam. Amina. KUTAKUWA NA MAKUNDI MATATU WATAKAOMWONA BWANA Kundi la kwanza ni laWafu waliolala katika Bwana au katika tumaini la kumlaki Kristo.Kundi la pili Watu waaminifu watakaokutwa wako hai juu ya uso wa nchi.Kundi la Tatu ni la watu maalumu la wenye dhambi hasa walimsulubisha pale msalabani watafufuliwa ili wamwone Yesu washuhudie maana aliwaahidi hili   kundi likiisha kumwona  wote watakufa tena MATHAYO 26:64
 V.            JE KUTAKUWEPO NA TETEMEKO LENYE KIWANGO GANI YESU ANAPORUDI?
Kutakuwepo na Tetemeko kubwa ambalo halijawahi kutokea katika historia ya mwanadamu UFUNUO 16:18 Pakawa na umeme na sauti na radi; na palikuwa na tetemeko la nchi kubwa, ambalo tangu wanadamu kuwako juu ya nchi hapakuwa namna ile, jinsi lilivyokuwa kubwa tetemeko hilo.
VI.            JE NI MAKUNDI MANGAPI YATAKAYOFUFULIWA WAKATI YESU ANAPORUDI?
1 WATHESALONOKE 4:13-18.  Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. Basi, farijianeni kwa maneno hayo.
KUTAKUWA NA MAKUNDI MAWILI
KUNDI LA KWANZA ni la watu waliokufa nalo limegawannyika mara mbili  moja ni KUNDI LA WAFU WALILALA KATIKA BWANA TU,kundi la pili ni KUNDI MAALUMU LA WENYE DHAMBI hasa ambao walimsulubisha Yesu msalabani MATHAYO 26:64 ambao ni Herode,watu waliomvika taji ya miiba, wale walisujudu mbele yake kwa dhihaka ya kukufuru,wale waliomtemea mate,wale waliompigilia misumari.hawa ndio watakaofufuliwa, kundi hili la waovu watakufa mara tatu yaani sasa hivi wameshakufa,Yesu anaporudi mara ya pili wafufuliwa kisha watakufa ,kwenye ufufuo wa pili wa waovu watafufuliwa tena kisha watachomwa moto  pamoja na waovu wengine
KUNDI LA PILI ni la watu watakaokutwa wako hai nalo limegawanyika mara mbili moja ni  watu wakakatifu ambao wataungana na wafu waliolala katika Bwana  watakaofufuliwa kisha watamraki Bwana mawinguni,kundi la pili ni watu waovu watakaokuwa hai hawa watamuona Yesu kisha watakufa UFUNUO 20:5
VII.            JE SANAMU AMBAZO LEO WANADAMU WANAZIABUDU ZITAWEZA KUWAOKOA ?
ISAYA 2:18-21 Nazo sanamu zitatoweka kabisa. Na watu wataingia ndani ya pango za majabali, na ndani ya mashimo ya nchi, mbele za utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake, atakapoondoka ili aitetemeshe mno dunia.Siku hiyo kila mtu atazitupilia mbali sanamu zake za fedha, na sanamu zake za dhahabu, walizojifanyia ili kuziabudu, kwa fuko na popo;
VIII.            JE MBINGU  HIZI TUNAZOZIONA ZITAKUWEJE  WAKATI YESU ANAPOKUJA?
UFUNUO 6;16 Mbingu zikaondolewa kama ukurasa ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake
IX.            JE KUNA UNYAKUO WA SIRI? JIBU HAPANA
MATHAYO 24:40-41 Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa; wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.FUNGU hili halimaanishi eti kutakuwa na unyakuo wa siri kwamba unashutukia tu mwenzako  hayupo tayari ameenda mbinguni hilo ni fundisho potofu Yesu anaporudi kila jicho litamwona.fungu hili humaanisha kuwa swala la wokovu ni la kila mmoja hatutaenda mbinguni kama familia,marafiki,kanisa bali kila mmoja atasimama peke yake.
MPENDWA USIKOSE SOMO LINALOFUATA  AMBALO LINASEMA KIFUNGO CHA SHETANI CHA MIAKA 1000
UKIWA NA SWALI ULIZA
 
 
 
 
 
 
 
 

,

No comments:

Post a Comment