a.
JE KIFUNGO HIKI KITACHUA MIAKA MINGAPI-JIBU ELFU
MOJA
UFUNUO 20:1-31 Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye
ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake. Akamshika yule joka, yule
nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu; akamtupa
katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa
tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda
mchache.
b.
JE NI KARAMU YA AINA GANI ITAFANYIKA KWA WAOVU
BAADA TU YA WATAKATIFU KWENDA MBINGUNI
UFUNUO
19:17-18 Kisha nikaona malaika
mmoja amesimama katika jua; akalia kwa sauti kuu, akiwaambia ndege wote warukao
katikati ya mbingu, Njoni mkutane kwa karamu ya Mungu iliyo kuu; mpate kula
nyama ya wafalme, na nyama ya majemadari, na nyama ya watu hodari, na nyama ya
farasi na ya watu wawapandao, na nyama ya watu wote, waungwana kwa watumwa,
wadogo kwa wakubwa
c.
JE MFUNGWA KATIKA KIFUNGO HIKI ATAKUWA NI
NANI–JIBU NI SHETANI NA MALAIKA ZAKE
UFUNUO
20:2 Na hiyo miaka elfu
itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake
d.
JE GEREZA LA SHETANI LITAKUWA WAPI HAPA DUNIANI Jibu
ni dunia yote itakuwa Gereza Lake
e.
JE BAADA YA KIFUNGO KUISHA NINI KITATOKEA?-
SHETANI ATAFUNGULIWA KWA MUDA KIDOGO TU
UFUNUO
20:7 Na hiyo miaka elfu
itakapokwisha, shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake
f.
JE SHETANI NA MALAIKA ZAKE WATACHA KAZI YA
UDANGANYIFU ?-JIBU HATAACHA
UFUNUO 20:8 Naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne
za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga
wa bahari
g.
JE SHETANI SHAMBULIO LAKE LA MWISHO NI LIPI ?
–JIBU NI ZIDI YA NGOME YA MUNGU
UFUNUO
20:8-9 naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne
za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga
wa bahari. Wakapanda
juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa.
Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala
h.
JE MWISHO WA SHETANI, MALAIKA ZAKE NA WATU
ALIOWADANGANYA UTAKUWAJE?–JIBU WATACHOMWA MOTO NA KUWA MAJIVU KABISA NA
HAWATAKUMBUKWA
UFUNUO
20:10 Na yule Ibilisi,
mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule
mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na
milele.
i.
ANGALIA NUKUU HII
KUTOKA KITABU CHA TUMAINI KUU KILICHAANDIKWA NA ELLEN G WHITE UK 402
KICHWA CHA HABARI ;MWISHO
MBAYA WA WAOVU
Tabia ya Shetani haijabadilika .kwa mara nyingine , uasi
kama mkondo wa maji yenye nguvu unaibuka .ataazimu kutoacha jitihada zake za
mwisho dhidi ya mfalme wa mbinguni
......EZEKIELI 28:6-8,16-19 nami nitakuangamiza
ewe kerubi ufunikaye utoke katika
mawe hayo ya moto ...nimekutupa chini ,nimekulaza mbele ya wafalme wapate kukutazama ... nami nimekufanya kuwa
majivu juu ya nchi,machoni pa watu
wote wakutazamao...umekuwa kitu cha
kutisha wala hautakuwepo tena hata
milele
Maana Bwana ana
ghadhabu juu ya mataifa yote
awanyeshee wasio haki mitego
,moto na kiberiti na upepo wahari
na viwe fungu la kikombe chao ISAYA 34:2 ZABURI 11:6.moto utashuka mbinguni kwa Mungu .dunia itavunjika .miali
ya moto ulao unateketeza utaibuka
kutoka kwenye miamba yenywe
itashika moto vitu vitaunguzwa kwa moto mkali ,Dunia pia na matendo yaliyomo humo yataunguzwa 2 petro
3:10.uso wa Dunia unaonekana
kama tope kubwa
ziwa kubwa la moto
ni siku ya kisasi cha bwana ,mwaka
wa malipo ili kushindania sayuni ISAYA 34:8
Waovu wanaadhibiwa sawasawa na matendo yao .Shetani
atateseka sio tu kwa uasi wake
lakini kwa dhambi zote alizosababisha watu wa mungu
kutenda .hatimaye katika moto
waovu wataangamizwa,mizizi na
tawi –shetani ndiye mzizi na wafuasi
wake ni matawi .adhabu kamili kwa
uasi wa sheria imekwisha kutolewa ;hitaji la haki
yamekwisha kutimizwa ,kazi ya
shetani ya uharibifu imekomeshwa milele
sasa viumbe wa Mumgu wamekombolewa milele kutoka kwenye majaribu yake
MPENDWA OMBA SANA ILI UOKOLEWE.USIKOSE SOMO LINALOFUATA
MAISHA YA WATAKATI KATIKA KIPINDI CHA MIAKA 1000
:
No comments:
Post a Comment