UFUNUO
21:1-2 Kisha nikaona mbingu mpya
na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita,
wala hapana bahari tena. Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya,
ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi
aliyekwisha kupambwa kwa mumewe
I.
Angalia jinsi mji mtakatifu Yerusalemu ulivyo
jengwa na unavyoonekana.
UFUNUO
21:10- 21 10 Akanichukua katika Roho mpaka mlima mkubwa, mrefu,
akanionyesha ule mji mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa
Mwenyezi Mungu; wenye utukufu wa Mungu, na mwangaza wake ulikuwa mfano wa kito
chenye thamani nyingi kama kito cha yaspi, safi kama bilauri; ulikuwa na ukuta
mkubwa, mrefu, wenye milango kumi na miwili, na katika ile milango malaika kumi
na wawili; na majina yameandikwa ambayo ni majina ya kabila kumi na mbili za
Waisraeli. Upande wa mashariki milango mitatu; na upande wa kaskazini milango
mitatu; na upande wa kusini milango mitatu; na upande wa magharibi milango
mitatu. Na ukuta wa mji ulikuwa na misingi kumi na miwili, na katika ile
misingi majina kumi na mawili ya wale mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo. Na yeye aliyesema nami alikuwa na
mwanzi wa dhahabu, apate kuupima huo mji, na milango yake, na ukuta wake. Na ule mji ni wa mraba, na marefu
yake sawasawa na mapana yake. Akaupima mji kwa ule mwanzi; ulikuwa kama maili
elfu na mia tano; marefu yake na mapana yake na kwenda juu kwake ni sawasawa.
Akaupima ukuta wake, ukapata dhiraa mia na arobaini na nne, kwa kipimo cha
kibinadamu, maana yake, cha malaika. Na majenzi ya ule ukuta wake yalikuwa ya
yaspi, na mji ule ulikuwa wa dhahabu safi, mfano wa kioo safi. Na misingi ya ukuta wa mji ilikuwa
imepambwa kwa vito vya thamani vya kila namna. Msingi wa kwanza ulikuwa yaspi;
wa pili yakuti samawi; wa tatu kalkedoni; wa nne zumaridi; wa tano sardoniki;
wa sita akiki; wa saba krisolitho; wa nane zabarajadi; wa kenda yakuti ya
manjano; wa kumi krisopraso; wa kumi na moja hiakintho; wa kumi na mbili
amethisto. Na ile milango kumi na miwili ni lulu kumi na mbili; kila mlango ni
lulu moja. Na njia ya mji ni dhahabu safi kama kioo kiangavu.
II.
kuna
masharti mawili ya huu
mji mtakatifu
Moja
hauhitaji jua wala mwezi ili kuuangaza mbili milango yake haitafungwa kamwe
UFUNUO 21:23,25 Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana
utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-Kondoo. . Na milango yake
haitafungwa kamwe mchana; kwa maana humo hamna usiku.
III.
Historia fupi baada ya miaka 1000 kumalizika.
Mwisho
wa miaka 1000 kristo atarudi Duniani
akisindikizwa na waliokombolewa na jeshi la malaika ,Atawaamuru waovu
waliokufa kufufuka ili wapokee hukumu yao.Watafufuka watakuwa hawahesabiki kama mchanga wa bahari ,wakiwa na dalili za
ugonjwa na mauti .tofauti ilioje baina
ya wale waliofufuliwa kwenye ufufuo wa
kwanza
Kila jicho
litakuwa limegeuka kuutazama utukufu wa Mwana wa Mungu
kwa sauti moja jeshi la waovu
litasema : amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la Bwana MATHAYO 23:39 si upendo utakaosababisha tamko hili ,nguvu ya ukweli italazimisha maneno kutoka kwenye midomo isiyoradhi kutamka kama ilivyokuwa wakati walipolala katika makaburi yao ,waovu watafufuliwa wakiwa na
uadui ule ule kwa Kristo wakiwa
na roho ile ile ya uasi .hawatapata kipindi kingine cha rehema
ili kurekebisha maisha yao yaliyopita
Nabii
anasema “Miguu yake itasimama juu ya
mlima wa MIZEITUNI nao mlima wa
mizeituni utapasuka katikati yake ZEKARIA 14:4 Yerusalemu Mpya utakaposhuka kutoka mbinguni , utakaa juu ya
mahali palipotayarishwana Kristo na waytu wake
na malaika wataingia kwenye Mji Mtakatifu
Akiwa amekatiliwa
mbali na kazi za udanganyifu ,mkuu wa uovu atakuwa
na huzuni na kuvunjika matumaini
,lakini waovu waliokufa
watakapofufuliwa na atakapouona
mkutano mkubwa ukiwa upande wake ,Matumaini yake yatakuwa hai .hakusudii kushindwa katika pambano kuu .atawapanga waliopotea
chini ya bendela yake. kwa kumkataa Kristo
waliukubali utawala wa mwasi ,walikuwa tayari kutimiza amri zake.akiwa
bado na hila zake za awali . atakataa
kukiri kuwa yeye ni shetani ,atadai kuwa yeye ndiye mmiliki halali wa Dunia
ambaye urithi wake ulinyanganywa pasipo
uhalali.atajionyesha mwenyewe kuwa ni mkombozi , akiwahakikishia wale
aliowadanganya kuwa ni uwezo wake
uliowafufua kutoka kutoka makaburini mwao ,shetani atawafanya waliodhaifu kuwa na nguvu
na atawavuvia wote kwa uwezo wake kuwaongoza kuutwaa mji wa Mungu ,
IV.
Shambulizi la mwisho dhidi ya Mungu
Shetani atashauriana
na watu hawa wenye nguvu.watasema kwamba jeshi lililo ndani ya mji
ni dogo likilinganishwa na la kwao na kwamba wataweza kushinda.mafundi
wenye ujuzi watatengeneza zana za vita
.viongozi wa kijeshi watapanga watu mapenda vita
katika makundi na vikosi
Hatimaye
amri ya kusonga mbele itatolewa na jeshi
lisilohesabika litasonga mbele ,jeshi hili litakuwa kubwa kiasi kwamba muungano
wa majeshi ya zama zote hautalingana nalo.shetani ataongoza kikosi
cha mstari wa mbele ,wafalme wa mashujaa wake
watakuwa kwenye msururu wake .kwa
umakini wa kijeshi wanajeshi wakiwa
wamejipanga kwenye mstari kulingana na
vyeo vyao .watasonga mbele juu ya uso wa nchi uliobomolewa,,wakiuelekea mji wa Mungu
.kwa amri ya YESu malango ya Yerusalemu Mpya yatafungwa na majeshi ya Shetani yatajipanga tayari kwa mapambano
V.
Hukumu yatolewa
dhidi ya waasi (hapa
kila mmoja ataonyeshwa maisha yake na
jinsi alivyomkataa kiristo)
kutawazwa
kwa Kiristo kutafanyika mbele ya mkutano
wa wakazi wa dunia na wa mbinguni .na sasa akiwa amevikwa enzi na nguvu
mfamle wa wafalme atatoa hukumu
kwa waasi ambao waliasi sheria na mfalme
wa wafalme atatoa hukumu kwa waasi
ambao waliasi sheria na kuwatesa watu wake ufunuo 20:11-12……
Macho
ya Yesu yatakapowaangalia waovu
,wataitambua kila dhambi ambayo waliwahi
kuitenda .wataona ni wapi miguu yao ilitanga pembeni mbali nanjia takatifui .majaribu yenye kushawishi ambayo
waliyawezesha kwa kuendekeza dhambi,wajumbe wa Mungu
waliopuuzwa,maonyo yaliyokataliwa ,mawimbi ya rehema yaliyorudishwa nyuma kwa ukaidi,moyo usiotubu yote
yataonekana kana kwamba
yaliandikwa kwa herufi za moto .Juu ya KITI
CHA ENZI MSALABA UTAINULIWA. kama kulivyo kuonekana kwa
SINEMA,yataonekena mazingira ya anguko
la ADAMU na hatua
zilizofuata za mpango wa ukombozi;(KWA
UFAFANUSI ZAIDI SOMA KITABU KILICHOANDIKWA NA ELLEN G WHITE CHA TUMAINI KUU ,SURA
YA 42)
Baada
ya kila mmoja muovu kujiona jinsi mbingu zilivyoshulikia wokovu wake ili
aokolewe lakini akakataa yeye mwenye kila mmoja atakili akisema MUNGU HUKUMU ZAKO NI ZA KWELI NA ZA HAKI na baada tu ya tukio la kukili linalofuata ni waovu kuchomwa
moto pamoja na SHETANI
UFUNUO 20:10 ;
SOMO LINALOFUATA
NI UNABII UNAOHUSU MAKANISA SABA.
No comments:
Post a Comment