Monday, December 19, 2016

MNYAMA WA NNE NI MWENYE KUTISHA-S/N 13



Na ufalme wa nne utakuwa na nguvu mfano wa chuma; kwa maana chuma huvunja vitu vyote na kuvishinda; na kama chuma kisetavyo vitu hivi vyote, ndivyo utakavyovunja-vunja na kuseta.  DANIELI 2:40 Baadaye nikaona katika njozi ya usiku, na tazama, mnyama wa nne, mwenye kutisha, mwenye nguvu, mwenye uwezo mwingi, naye alikuwa na meno ya chuma, makubwa sana; alikula na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake; na umbo lake lilikuwa mbali kabisa na wale wa kwanza, naye alikuwa na pembe kumi DANIELI 7:7

       I.            SABABU ZINAZOFANYA MNYAMA HUYU WA NNE KUTISHA SANA NA KUTOFANANA NA WANYAMA WENGINE WALIOTANGULIA NI HIZI

Alikuwa mwenye nguvu/Alikuwa na uwezo mwingi/ Alikuwa na meno ya chuma makubwa sana alikula na kuvunja vunja vipande vipande/Alikuwa na pembe kumi/Ulikuwa utawala wenye Utajiri /katili na kila aina ya maonevu  

     II.            MNYAMA HUWALIKISHA –Falme  au Ufalme DANIELI 7:17


III.            HABARI NJEMA NYINGINE TUNAYOIPATA HAPA - Katika utawala huu YESU ALIZALIWA katika utawala huu WA RUMI YA UPAGANI


 IV.            MNYAMA WA NNE WA KUTISHA NA MADINI YA CHUMA- Huwakilisha utawala wa RUMI YA UPAGANI hii ilikuwa ENZI  KUU YA NNE ULIMWENGUNI


    V.            PEMBE KUMI ALIZOKUWA NAZO MNYAMA HUYU WA KUTISHA -Zinawakilisha mgawanyiko wa DOLA YA RUMI YA UPAGANI katika majimbo kumi ambazo ni falme kumi


 VI.            DOLA HII YA RUMI YA KIPAGANI ILIANZA KUTAWA  ULIMWENGU -Tangu mwaka 168 B.C hadi 476A.D


VII.            IFUATAYO NI HISTORIA FUPI

 RUMI YA KIPAGANI  ilikuwa  ufalme  wenye nguvu  ulimwenguni  kuliko falme zingine zote  zilizotangulia .vilevile  Rumi ilitawala sehemu kubwa ya uso wa dunia kuliko falme zo zote zilizotangulia ikaunganisha sehemu za AFRIKA,ASIA,ASIA NDOGO NA ULAYA

Ufalme wa nne  ambao kwao hakuna mnyama aliyeumbwa kwa kutisha anayetosha kufananishwa nao Rumi ilifananishwa katika sura  ya pili  na Miguu ya chuma.Pembe kumi  ambazo ziliondoka  katika  maanguko  ya ufalme wa  Warumi ……...kuonea watu bure kulikuwa  kamili katika siku za Warumi …..kamwe hapakuwapo ulimwenguni  ufalme usio na huruma wenye  mamlaka hivi .Ulikizaja kikombe chake  cha udhalimu  kwa kushiriki katika  kusulubiwa kwa mwana wa  MUNGU na kuwaua wakristo wa kwanza

VIII.            NAKUOMBA mpendwa usikose  somo linalofuuta linalosema pembe

kumi na pembe moja iliyokua zaidi ikawa na nguvu kuliko zingine pia kumbuka katika utawala huu wa nne YESU KRISTO alizaliwa  na baadaye alipomaliza  kazi yake  alirudi mbinguni mada hii ya kuzaliwa kwa Yesu tutajifunza sana tutakapofika danieli sura ya 9.Mungu akubariki sana:

 

 

 

 

No comments:

Post a Comment