Mpendwa
katika Bwana tunaenda kujifunza UNABII wa DANIELI sura
ya PILI na
sura ya SABA
nakuomba ufuatilie MNYAMA mmoja hadi mwingine.
I.
LENGO LA KUJIFUNZA SURA YA PILI NA YA SABA NI HILI
SANAMU
YA SURA
YA PILI - Inaeleza historia ya
dunia kwa namna ihusuyo tu serikali za nchi ;MAONO YA SURA YA SABA ni
mfano wa falme nne za dunia katika
mambo ya maana ya kiroho kama
yalivyoelezwa kwa kazi ya MUNGU na watu
wake;
MNYAMA
WA KWANZA NI SIMBA- Alifananishwa na madini ya dhahabu (Danieli akanena, akisema, Naliona katika maono yangu
wakati wa usiku; na tazama, hizo pepo nne za mbinguni zilivuma kwa nguvu juu ya
bahari kubwa.Ndipo wanyama wakubwa wanne wakatoka baharini, wote wa namna
mbalimbali.Wa kwanza alikuwa kama SIMBA, naye alikuwa na mabawa ya tai; nikatazama, hata mabawa
yake yakafutuka manyoya, akainuliwa katika nchi, akasimamishwa juu kwa miguu
miwili kama mwanadamu; naye akapewa moyo wa kibinadamu. DANIELI
7:2-4 Hii ndiyo ile ndoto, nasi tutaihubiri tafsiri yake mbele
ya mfalme. Wewe, Ee mfalme, u mfalme wa wafalme, na Mungu wa mbinguni amekupa
ufalme, na uwezo, na nguvu, na utukufu; na kila mahali wakaapo
wanadamu, wanyama wa kondeni na ndege wa angani amewatia mkononi mwako, naye
amekumilikisha juu ya hao wote; wewe u kichwa kile cha dhahabu
DANIELI 2:36-38)
II.
MNYAMA ANAWAKILISHA NINI? DANIELI 7:17
Wanyama hao wakubwa walio wanne ni wafalme wanne
watakaotokea duniani.
JIBU
MNYAMA ANAWAKILISHA- Falme mbalimbali zitakazotokea Duniani
III.
KWA NINI WANYAMA HAWA WALITOKEA BAHARI AU
MAJINI?
JE MAJI
YANAWAKILISHA NINI UFUNUO 17:15
Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule
kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha.
JIBU
MAJI HUWAKILISHA -Jamaa na Makutano na Mataifa na Lugha
IV.
SIMBA NA DHAHABU iliwakilisha Enzi kuu ya kwanza
kutawala Ulimwengu au Dunia
V.
MABAWA YA TAI aliyokuwa nayo simba huonyesha
wepesi wa ushindi wa Babeli
VI.
MADINI YA DHAHABU yaliwakilisha utajiri ,uwezo
na utukufu mwingi uliokuwa Babeli
VII.
UTAWALA huu ulinza mnamo mwaka wa 605 B.C—538 B.C
VIII.
Wafalme waliotawala ENZI KUU YA KWANZA aliitwa
NEBUKADREZA alitawala miaka arobaini
na mitatu.alirithiwa na wafalme watano wadhaifu
sana ambao wa mwisho ndiye
BELISHAZA (tazama sura ya 5)
IX.
IFUATAYO NI HISTORI FUPI YA
Enzi
kuu ya kwanza kutawala ulimwengu
UFALME
wa Babeli ulianzishwa na NIMRODI kwa
kumwasi Mungu (Mwanzo 10:8-10) ulizidi kukua katika siku za
NEBUKADREZA,ukawa ufalme wenye
utajiri na utukufu mwingi katika ulimwengu.Nebukadreza mjenzi mstadi aliupamba mji huu mkuu kwa matengenezo yasiyo yakawaida baadaye twamsikia akisema mji huu sio babeli
mkuu nilioujenga mimi?( Danieli 4:30)
ulikuwa mji wa ajabu katika ulimwengu wa
kale pia ufalme wa kwanza simba huleta jawabu katika kichwa
cha dhahabu cha sanamu ya sura ya
pili ambao ulikuwa ufalme wa babeli
yeremia alibashiria Yuda kuja kwa jeshi
la Babeli kushambulia akiwafananisha na
kuja kwa simba mwenye kuangamiza Yeremia
4:7, 21:7 mabawa huonyesha wepesi wa jeshi wa babeli Habakuki 1:6-8 alisema ya
kwamba farasi wa wakaldayo ni wepesi
kuliko chui………… huruka kama tai afanyae
haraka ale
Lengo
lingine la kujifunza unabii huu utatusaidia kujua hiStoria yetu kwamba tumetoka
wapi na tunaenda wapi ili tujue tuchukue tahadhali dhidi ya mafundisho ya uongo
X.
Pia kupitia historia hii ya falme mbalimbali
tutajifunza historia ya Makanisa mbalimbali kwamba yametoka wapi kwa nini leo
ni mengi sana na kila kanisa hudai liko sahihi je ni kweli?
XI.
Mpendwa fuatilia kwa makini utajua tu usikose
hata somo moja Mungu akubariki SOMO LA
PILI LITAHUSU MNYAMA DUBU USIKOSE
No comments:
Post a Comment