Monday, December 19, 2016

PASAKA YA KWELI INAYOFUATA HATUA TATU:-S/N 7

KATIKA SOMO HILI TUNAJIFUNZA VIPENGELE VITANO;

          i.            PASAKA NINI?

Pasaka ilikuwa imeanzishwa kuwa ukumbusho wakukombolewa kwa waisraeli kutoka katika utumwa wa Misri.

       ii.            CHAZO  AU CHIMBUKO LA PASAKA

 
kila mtu atatwaa mwakondoo…tena mtamla hivi  mtakuwa  mmefungwa  viuno vyenu , mmevaa viatu vyenu  miguuni ,na fimbo zenu mikononi  mwenu  nanyi mtamla kwa haraka  ni pasaka kwa bwana KUTOKA 12:3

 iii.            ZIFUATAZO NI HATUA TATU AMBAZO KILA MTU ANAYEAZIMISHA  PASAKA ANAPASWA  KUZIFUATA;

HATUA YA KWANZA NI KUTAWAZANA MIGUU ;YOHANA 13 :1-15

Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika,...........  aliondoka chakulani; akaweka kando mavazi yake, akatwaa kitambaa, akajifunga kiunoni. Kisha akatia maji katika bakuli, akaanza kuwatawadha wanafunzi miguu, na kuifuta kwa kile kitambaa alichojifunga........... Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu, nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo kutawadhana miguu ninyi kwa ninyi. sababu kubwa ya kutawaza miguu ni hii hapa

Katika moyo wa mwanadamu  kuna hali  ya kujitukuza  mwenyewe na kujiona kuwa bora kuliko mwenzake;kujipendelea ,kutafuta ukuu; na mara nyingi  huwa na matokeo ya dhana potovu na chuki.huduma ya kutawazana  inayotangulia meza ya bwana  inakusudiwa kumwondoa mtu katika ubinafsi,kumshusha kutoka katika kujiinua nafsi,na kumleta katika unyenyekevu utakaomwezesha kumhudumia ndugu yake  mwonaji Mtakatifu kutoka  mbinguni  huwapo katika huduma hii  kuifanya kuwa ya  kutafakari mambo ya kiroho kujutia dhambi.kristo huwapo kubadilisha mkondo wa mitiririko wa mawazo ya ubinafsi

HATUA  YA PILI  KUNYWA DIVAI ;LUKA 22:17,201

Akapokea kikombe, akashukuru, akasema, Twaeni hiki, mgawanye ninyi kwa ninyi;  Kikombe nacho vivyo hivyo baada ya kula; akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, inayomwagika kwa ajili yenu.]

HATUA YA TATU NI KULA MKATE  LUKA 22:19

Akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa, akisema, [Huu ndio mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.        

     iv.            NINI MAANA YA MEZA YA BWANA AU PASAKA  AMBAYO YESU ALISHIRIKI?

Meza ya Bwana ilianzishwa kuwa ukumbusho wa kukombolewa kulikoletwa kama matokeo ya kifo cha kristo adhimisho la agizo hili ndiyo njia ya kutukumbusha daima kazi yake kuu kwa ajiri ya wokovu wetu

SABABU YA KUAZIMISHA MEZA YA BWANA

Lakini huduma ya meza ya Bwana haikukusudiwa kuwa wakati wa huzuni .kadiri wanafunzi wa Yesu watapokusanyika mezani pa Bwana hawapaswi kuomboleza kwa ajiri ya upungufu wao. hawapaswi kutafakari tofauti zao  na wenzao  huduma ya kutawazana  imeshugulikia yote hayo .sasa wanakuja kukutana  na kristo,hawapaswi kusimama kwenye kivuli cha msalaba  bali katika mwanga wake wa wokovu,wanapaswa kufungua mioyo yao kwa  nuru itokayo jua lakini  wanapaswa kusikia maneno yake

        v.            WANAORUHUSIWA KUSHIRIKI

 katika pasaka ni watu wote  waliobatizwa kwa maji mengi Watu ambao hawaruhusiwi kushiriki pasaka ni wale walioondolewa kwenye vitabu  vya ushirika au vya kanisa kutokana na  kutenda dhambi ya kulidhalilisha kanisa hadi hapo watakapobatizwa tena Watu wengine wasioruhusiwa ni watoto na watu wazima ambao hawajabatizwa .

TAHADHALi mpendwa kama hizo hatua tatu hushiriki wakati wa kuazimisha pasaka jua kabisa pasaka unayoazimisha siyo sahihi chukua hatu pia pasaka ya Bwana siyo ya kuchinja ngome ,kuku,mbuzi ,kushona nguo, na mengineyo

 

 

 

 

 

 

 

 

No comments:

Post a Comment