Monday, December 19, 2016

KWA NINI POMBE IMEKATAZWA NA MUNGU?-S/N 9



HABAKUKI 2:15 :Ole wake  yeye ampaye jirani yake kileo ,wewe utiaye  sumu yako,na kumlevya  pia ,ili kuutazama uchi wao

      I.            UNYWAJI WA POMBE KWA MARA YA KWANZA KATIKA HISTORI YA MWANADAMU,MWANZO 9:20-21

Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu; akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake

Nuhu: Akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake

   II.            ORODHA YA MADHARA  YANAYOTOKANA  NA MATUMIZI YA POMBE MITHALI 23:29-35,

 Ni nani apigaye, Yowe? Ni nani aliaye, Ole? Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani mwenye mguno? Ni nani aliye na jeraha zisizo na sababu? Ni nani aliye na macho mekundu?  Ni wale wakaao sana kwenye mvinyo; Waendao kutafuta divai iliyochanganyika. Usiitazame mvinyo iwapo ni nyekundu; Iitiapo bilauri rangi yake, ishukapo taratibu; Mwisho wake huuma kama nyoka; Huchoma kama fira.  Macho yako yataona mambo mageni; Na moyo wako utatoa yaliyopotoka. Naam, utakuwa kama alalaye katikati ya bahari; Au kama yeye asinziaye juu ya mlingoti.Utasema, Wamenichapa wala sikuumia; Wamenipiga wala sina habari; Nitaamka lini, nitazidi kuitafuta tena. Mithali 20:11 Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi; Na akosaye kwa vitu hivyo hana hekima

III.            JE KUNA MTU YOYOTE ANAYERUHUSIWA KUNYWA  POMBE WAEFESO 5:18,

 Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho

Walawi 10:9 Usinywe divai wala kileo cho chote, wewe, wala wanao pamoja nawe, hapo mwingiapo ndani ya hema ya kukutania, ili kwamba msife; amri hii itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyenu;


IV.            JE WATUMISHI WA MUNGU WANARUHUSIWA KUNYWA POMBE ISAYA 28:7

Lakini hawa nao wamekosa kwa divai, wamepotea kwa kileo; kuhani na nabii wamekosa kwa kileo, wamemezwa kwa divai, wamepotea kwa kileo; hukosa katika maono, hujikwaa katika hukum,Isaya 56:10-12Walinzi wake ni vipofu, wote pia hawana maarifa; wote ni mbwa walio bubu, hawawezi kulia; huota ndoto, hulala, hupenda usingizi. Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote. Husema, Njoni, nitaleta divai, Na tunywe sana kileo; Na kesho itakuwa kama leo, Sikukuu kupita kiasi.


   V.            JE MUNGU ANATOA OLE GANI  KWA WATUMIAJI WA POMBE

 ISAYA 5:11 ,22

Ole wao waamkao asubuhi na mapema, wapate kufuata kileo; wakishinda sana hata usiku wa manane mpaka mvinyo imewaka kama moto ndani yao Ole wao walio hodari kunywa kileo chenye nguvu, watu waume wenye nguvu kuchanganya vileo


VI.            JE MUNGU ANASEMAJE JUU YA WATU WOTE WANAOTUMI POMBE WAGALATI 5:19-21

Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu

Katika kitabu kilichoandikwa na Ellen g white

 KUTAYARISHA NJIA SEHEMU YA KWANZA, SURA 16 NJIA KUU YA SHETANI KULETA UHARIBIFU, UK 117-121 ANASEMA

Shetani aliwakusanya malaika wabaya pamoja kutafuta njia ya kufanya uovu mkubwa  iwezekanavyo kwa wanadamu.mashauri yakatolewa moja moja ,mpaka mwishowe shetani mwenyewe akafikiri njia .akapenda kuyatwaa matunda ya mzabibu ,pia ngano na vitu vingine vilivyotolewa na Mungu  chakula  na kuvigeuza kuwa sumu  ambayo ingeuharibu uwezo wa mwanadamu wa mwili ,akili ,na tabia ya moyoni na hivyo atazishinda akili za kupambanua mema na mabaya hata shetani apate kutawala kabisa.,,,,,,,,,,,kwa mvuto  wa kinywaji wanywacho watu huongozwa kutenda mambo  ambayo kama wasingelikuwa  wameonja kitu  chenye kulevya  na kurusha akili  wangeepuka kwa hofu kuyatenda wakiwa katika hali ya kulewa  wako kwenye mamlaka ya shetaninao husaidiana naye    DIVAI ambayo kristo aliifanyia kwa maji katika karamu ya arusi ya kana ilikuwa majimaji matupu ya zabibu.

 

 

 

No comments:

Post a Comment