Mpendwa ulinzi huu ni wa peke
yake:Bwana asipoilinda nyumba/ mji wako
walindao wanakesha bure.
JIFUNZE JINSI ULINZI WA MUNGU
ULIVYO
i.
USIOGOPE
ISAYA 41:10-13, ISAYA 59:1
Usiogope,
kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam,
nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.Tazama, wote
walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe
watakuwa si kitu, na kuangamia. Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe;
watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu
yako. Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume,
nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia.
ii.
WALINZI WETU NI MALAIKA WA MUNGU
ZABURI 91:11-12,34:7, WAEBRANIA
1:14 Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia
zako zote. Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe
iii.
HUPASWI
KUHOFU SHAMBULIO LOLOTE LIWE LA GHAFULA
AU SIO
ZABURI 91:5-10 Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana Wala tauni
ipitayo gizani, Wala uele uharibuo adhuhuri, Ijapo
watu elfu waanguka ubavuni pako. Naam, kumi elfu mkono wako wa kuume! Hata
hivyo hautakukaribia wewe. Ila kwa macho yako utatazama, Na kuyaona malipo ya
wasio haki. Kwa kuwa Wewe Bwana ndiwe kimbilio langu; Umemfanya Aliye juu kuwa
makao yako. Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako
iv.
UKIMWAMINI MUNGU ULINZI WA MUNGU NI WA HAKIKA
SOMA MIFANO HII
2 WAFALME 6:13-23- SOMA hili
fungu lote utaona Elisha avyopambana na jeshi la watu wengi na kushinda kwa
kishindo kikubwa
DANIELI 6:18-24 -SOMA utaona Danieli
alivyoshinda japokuwa walimtupa kwenye tundu la simba ili auawe na simba
TAHADHALI usiwategemee wanadamu /wala mazindiko ya uganga
/uchawi aina yoyote . maana vitu kama hivyo kwa Mungu havifanyi kazi
yoyote.YEREMIA 17:5-Bwana asema hivi,
Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake
Na moyoni mwake amemwacha Bwana.
No comments:
Post a Comment