Monday, December 26, 2016

MIAKA ELFU MOJA YA WATAKATIFU MBINGUNI;S/N 19




JE MBINGUNI NI MAHALI HALISI-JIBU NDIO

YOHANA 14:1-3, Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo. WAEBRANIA 11:16 Lakini sasa waitamani nchi iliyo bora, yaani, ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni haya kuitwa Mungu wao; maana amewatengenezea mji.

VITU AU MAMBO YATAYOKUWA YANAENDELEA MINGUNI BAADA YA WAKATIFU KUFIKA

          i.            WAKATIFU WATAKAPOFIKA MBINGUNI WATAKARIBISHWA NA YESU

 Mathayo 25:34 Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu

       ii.            YESU ATAWAVISHA TAJI YA USHINDI

Watapewa taji ya uzima “thawabu yaani, utukufu ule wa mbinguni, watakaopewa washindi wale, italingana na kiwango walichoweza kuiwakilisha TABIA YA KIRISTO katika Ulimwengu huu..Taji ya Uzima itangaa sana  au itakuwa na mwanga  uliofifia ,itametameta ikiwa  na nyota nyingi,au itaangazwa kwa johari chache sana ,kulingana na mwenendo wetu wenyewe(OHC 123) ,2 WAKORINTHO 9:6 Lakini nasema neno hili, Apandaye haba atavuna haba; apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu.

     iii.            WATAKATIFU WATAFANYIWA KARAMU KUBWA YENYE VINONO

ISAYA 25:66 Na katika mlima huu Bwana wa majeshi atawafanyia mataifa yote karamu ya vitu vinono, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, karamu ya vinono vilivyojaa mafuta, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, iliyochujwa sana.

     iv.            KAZI MOJAWAPO WATAKAZOKUWA WANAZIFANYA WATAKATIFU NI KUPITIA HUKUMU AMBAZO YESU AMEKWISHA KUZITOLEA MAAMUZI,HUO NDIO UTAKUWA WAKATI WAKUTAMBUANA KWA NINI FURANI HAKUOKOLEWA

1 WAKORINTHO 6:2-3 Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya UFUNUO 20:4-6Kisha nikaona viti vya enzi, wakaketi juu yake, nao wakapewa hukumu; nami nikaona roho zao waliokatwa vichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu. , (1 WAKORINTHO 4:5)

        v.            WATU WATAKUWA NA MAUMBILE GANI?

Urefu  wa karibu  futi kumi na mbili” wakiwa wemerejeshwa kwenye mti wa uzima  katika edeni ile iliyopotea zamani  sana wale waliokombolewa  wataendelea kukua (malaki 4:2) na kufikia kimo kamili  cha  jamii  ya wanadamu wa asili katika utukufu wake (gw 676) yeye adamu alikuwa na erefu  wa zaidi ya mara  mbili kuliko  ule  wa mwanadamu wanaoishi sasa na mwili wake  uliumbika ukiwa na uwiano mzuri

  vi.            JE MAUMIVU, KIFO YATAKUWAPO?

Maumivu hayawezi kuwako katika mazingira yale ya mbinguni .hapatakuwepo na machozi tena ,wala misafara  ya mazishi ,wala tepe za maombolezo ,wala kilio..kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita ,wala hapana mwenyeji  atakayesema  mimi  mgonjwa ( UFUNUO 21:4,ISAYA 33:24),(GW 676)

   vii.            JE KUMBUKUMBU ZAO ZITAKUWEJE

Kumbukumbu zetu zitakuwa kamili kabisa watu wale  walioishi kabla ya gharika  walikuwa  hawana vitabu  hawakuwa na kumbukumbu zote zilizoandikwa ,lakini wakiwa wenye nguvu  nyingi za kimwili na kiakili ,walikuwa na kumbukumbu zao thabiti ,zenye uwezo wa kunasa kile walichokuwa  wameambiwa ,nao kwa zamu yao  kuweza  kuwapa wazao wao  bila kuuathiri ujumbe ule

viii.            JE MACHO YAO YATAKUWA NA UWEZO GANI?

Watakuwa na macho  kama DARUBINI  yaonayo vitu vidogo sana na vile  vilivyo mbali sana  kwa macho  yaonayo wazi  kabisa  wataangaza na  kuungalia  utukufu wa uumbaji

  ix.            JE UWEZO WAO WA KUSAFIRI UTAKUWAJE?

Uwezo wa kusafili katika anga msongamano wa waliokombolewa utazunguka toka Dunia moja  kwenda Dunia  nyingine na wakati wao mwingi utatumika  katika kuzichunguza siri za ukombozi

       x.            JE KUTAKUWA NA MAISHA YA KIFAMILIA, NDOA NA KUZAA WATOTO KULE?

Hakuna ndoa kule wala kuzaa watoto kuna watu leo wanaoeneza imani yao  wakisema  kwamba kutakuwa  na ndoa  na kuzaa watoto katika nchi mpya ,lakini basi  ,wale wanaoyaamini maandiko  hawawezi kulikubali fundisho  kama hilo ,fundisho linalosema  kwamba  watoto watazaliwa katika nchi mpya  halina sehemu   katika  lile  neno la unabii lililo imara zaidi (MM99,1SM 172) MATHAYO 22:23-30

  xi.            NI KUMBUKUMBU GANI MOJA PEKEE YA KAZI YA KIKATILI ILIYOFANYWA NA DHAMBI AMBAYO ITAKUWA MBELE DAIMA?

Kumbukummbu moja pekee itabaki: mkombozi wetu daima  atachukua  alama  zile za kusulubiwa  kwake . Juu ya kichwa chake  kilichojeruhiwa ,ubavu ni pake ,katika viganja  vyake  vya mikono  na miguu ,hizo ndizo alama pekee za kazi  ya kikatili  ambayo  dhambi  imefanya kwake(gw)

 

  xii.            JE MBINGUNI KUTAKUWA NA IBAADA?-JIBU NDIO

Kukusanyika pamoja kumwabudu Mungu. Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na SABATO HATA SABATO, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana.

xiii.            JE NI MASOMO YAPI WATAJIFUNZA WATAKATIFU

Baadhi ya masomo wakayojifunza ni haya watajifunza HISTORIA YA PAMBANO KUU ,kugundua SABABU YA MATATIZO YOTE YA MAISHA HAYA  ,KUJIFUNZA USHINDI WA KILA TENDO JEMA NA BAYA  KATIKA MAISHA HAYA  WATATUNGA NYIMBO NA KUSILIZA  MUZIKI ULE ULIO MKAMILIFU SANA na mengineyo

MPENDWA USIKOSE jitahidi ukaone mwenyewe somo linalofuata mji MPYA YERUSALEMU UKISHUKA KUTOKA MBINGUNI usikose.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

       

 

No comments:

Post a Comment