KAMA JIBU
NI NDIYO AU HAPANA ZINGATIA YAFUATAYO .
I.
CHANZO CHA
UADUI NI MAKWAZO YANAYOTOKANA WATU MBALIMBALI
Akawaambia
wanafunzi wake, Makwazo hayana budi kuja, lakini ole wake mtu yule ambaye yaja
kwa sababu yake! Ingemfaa
zaidi mtu huyo jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake, akatupwe baharini,
kuliko kumkosesha mmojawapo wa wadogo hawa.LUKA 17:1-2
II.
MPENDE
ADUI YAKO
Mmesikia
kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako; lakini mimi
nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi.MATHAYO 5:43-45, 1 WAKORINTHO13:4-8
III.
MWOMBEE
ADUI YAKO
lakini
mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi, ili mpate kuwa wana wa Baba yenu
aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua
wenye haki na wasio haki.MATHAYO
5:44-45
IV.
USIMFANYIE
ADUI YAKO JAMBO BAYA
Pendo
halimfanyii jirani neno baya; basi pendo ndilo utimilifu wa sheria WARUMI 13:10
V.
USIWE NA UPENDO WA KINAFIKI AU MCHONGEZI KWA ADUI YAKO
Pendo na
lisiwe na unafiki lichukieni lililo ovu, mkiambatana na lililo jema.WARUMI 12:9. Usiende huko na huko
katikati ya watu wako, kama mchongezi; wala usisimame kinyume cha damu ya
jirani yako; mimi ndimi Bwana.WALAWI
19:16
VI.
USILIPIZE KISASI WALA KUWA NA KINYONGO
Usimchukie
ndugu yako moyoni mwako; ni lazima kumkemea jirani yako, wala usichukue dhambi
kwa ajili yake. Usifanye kisasi, wala kuwa na
kinyongo juu ya wana wa watu wako; bali umpende jirani yako kama nafsi yako;
Mimi ndimi Bwana WALAWI19:17-18. Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni
pa watu wote. Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote Wapenzi, msijilipize
kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu
mimi; mimi nitalipa, anena Bwana.WARUMI
12:17-19
KANUNI YA
MUNGU KWA WALIPA KISASI MITHALI 17:13
Yeye
arudishaye mabaya badala ya mema, Mabaya hayataondoka nyumbani mwake
VII.
NAMANA YA
KUSHUGHURIKIA MAKWAZO
Na ndugu yako akikukosa, enenda ukamwonye,
wewe na yeye peke yenu; akikusikia, umempata nduguyo. La, kama hasikii, chukua
pamoja nawe tena mtu mmoja au wawili, ili kwa vinywa vya mashahidi wawili au
watatu kila neno lithibitike. Na asipowasikiliza wao,
liambie kanisa; na asipolisikiliza kanisa pia, na awe kwako kama mtu wa mataifa
na mtoza ushuru. MATHAYO 18:15-19
VIII.
USIFURAHI
WALA USIKASILIKE ADUI YAKO ANAPOJIKWAA
Kwa maana
mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na
mabaya.Usifurahi, adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo Bwana asije akaliona
hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake. Usikasirike kwa sababu
ya watenda mabaya; Wala usiwahusudu wabaya; Kwa maana mtu mbaya hapati thawabu;
Taa ya mtu mbaya itazimika.MITHALI
24:16-20
IX.
UWE TAYARI
KUTOA MSAMAHA USIO NA MASHARTI
Jilindeni;
kama ndugu yako akikosa, mwonye; akitubu msamehe. Na kama akikukosa mara saba
katika siku moja, na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe.LUKA 17:3-4.Kisha
Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami
nimsamehe? Hata mara saba? Yesu akamwambia, Sikuambii hata
mara saba, bali hata saba mara sabini.MATHAYO
18:21-22.Nanyi, kila msimamapo na
kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni
awasamehe na ninyi makosa yenu.Lakini kama ninyi hamsamehe, wala Baba yenu
aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.MARKO11:25-26
X.
KUWABARIKI
WANAOKUUDHI
Wabarikini
wanaowaudhi; barikini, wala msilaani.WARUMI
12:14
XI.
MHUDUMIE
ADUI YAKO
Lakini,
Adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe; maana ufanyapo hivyo,
utampalia makaa ya moto kichwani pake. Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya
kwa wema.WARUMI 12:20-21.Yeye asemaye kwamba yumo nuruni, naye amchukia ndugu
yake, yumo gizani hata sasa.Yeye ampendaye ndugu yake, akaa katika nuru, wala
ndani yake hamna kikwazo. Bali yeye amchukiaye ndugu yake, yu
katika giza, tena anakwenda katika giza, wala hajui aendako, kwa sababu giza
imempofusha macho.1 YOHANA 2:?9-11
TAHADHALI
kama
kuna mtu amekukosea na wewe hutaki kumsamehe na unatunza vinyongo na visasi
moyoni mwako ujue kabisa ibaada yako ni
ya bure,maana hata Mungu naye hatakusamehe wewe pia MARKO 11:25-26 Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na
neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa
yenu. Lakini
kama ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa
yenu
No comments:
Post a Comment