Monday, December 26, 2016

UNABII WA MUHURI SABA NI SAWA NA UNABII WA MAKANISA ;S/N 23


UFUATAO NI MCHANGANUO WAKE

UFUNUO 6:1 Kisha nikaona napo Mwana-Kondoo alipofungua moja ya zile muhuri Saba, nikasikia mmoja WA wale wenye uhai wanne akisema, Kama Kwa sauti ya ngurumo, Njoo

JE MUHURI SABA INAWAKILISHA NINI?-MUHURI SABA Inatuleta ama katika ushindi wenye utukufu au katika kushindwa kunakotisha katika ibaada ya utukufu ya kuja kwa YESU.

JE FARASI HUWAKILISHA NINI?- FARASI NI mfano wa wajumbe wa MUNGU wajumbe waliotumwa kuleta vyote wokovu na hukumu.

MUHURI WA KWANZA.(kanisa la Efeso)

 FARASI MWEUPE.

UFUNUO 6:2 Nikaona, Na tazama, farasi mweupe, Na yeye aliyempanda ana uta, akapewa taji, naye akatoka, ali akishinda tena apate kushinda

MAANA YA KWANZA YA FARASI MWEUPE-Farasi mweupe Ni mfano wa kuhesabiwa haki na ushindi.

MAANA YA PILI YA FARASI MWEUPE-Farasi mweupe Ni barabara ya kufaulu injili katika karne ya kwanza ya historia ya Ukristo, hii ilikuwa mfano wa kanisa la Mitume sawa na MFANO WA KANISA LA EFESO katika Ufunuo 2:1

UTA UNAMAANISHA NINI?-Uta katika mkono ni uhakikisho wa ROHO Mtakatifu katika mioyo ya wanadamu.Maneno ya mitume yalikuwa makali Kama mishale ya Mwenyezi yakithibitishia wadhambi uovu wa kutisha katika kukataa na kumsubisha Bwana wa utukufu.

MUHURI WA PILI (kanisa Smirna)

FARASI MWEKUNDU.

UFUNUO 6:3-4 Na alipoifungua muhuri ya pili, nikamsikia yule mwenye uhai wa pili akisema, Njoo!  Akatoka farasi mwingine, mwekundu sana, na yeye aliyempanda alipewa kuiondoa amani katika nchi, ili watu wauane, naye akapewa upanga mkubwa

FARASI MWEKUNDU HUWAKILISHA NINI ?–Ni mfano wa mauaji na mateso waliofanyiwa wafuasi wa YESU baada ya wakati wa Mitume ambacho ndicho kipindi cha KANISA LA SMIRNA KATIKA UFUNUO 2:8

MUHURI WA TATU.( kanisa la pergamo)

FARASI MWEUSI

UFUNUO 6:5-6 Na alipoifungua muhuri ya tatu, nikamsikia yule wa tatu mwenye uhai akisema, Njoo! Nikaona, na tazama, farasi mweusi, na yeye aliyempanda ana mizani mkononi mwake. Nikasikia kama sauti katikati ya hao wenye uhai wanne, ikisema, Kibaba cha ngano kwa nusu rupia, na vibaba vitatu vya shayiri kwa nusu rupia, wala usiyadhuru mafuta wala divai

FARASI MWEUSI  ALIWAKILISHA NINI?-Aliwakilisha hali za watu wa MUNGU zilikuwa zinaendelea kuwa ngumu kwanza .FARASI MZURI MWEUPE akiwa mfano wa usafi  na ushindi halafu MWEKUNDU sana ni mfano wa mateso  na kisha sasa mfano wa kutisha wa njaa( farasi huyu MWEUSI nawakilisha  kuwa ne no la Mungu liliadimika siku  hizo za kanisa la pergamo)

SAUTI ILIYOTANGAZA HABARI MBAYA  kibaba cha ngano au shayiri kilikuwa ndicho posho ya kila kila siku kama vile ratili moja na nusu ya unga  wa mahindi wakati mwingine unafikiliwa  kilikuwa chakula cha kila siku cha askari wa kiafrika.RUPIA katika nyakati za agano jipya  ilikuwa ndiyo ujira wa kibarua kwa siku nzima (Mathayo 20:1,20)

PERGAMO CHA UFUNUO 2:12 Hekaya za kupendeza na mapokeo ya wanadamu yalilisonga mno neno la Mungu wale waliokwenda kanisani walipata chakula haba cha kulisha roho zao

Nakala za biblia zikawa adimu kiasi kidogo tu cha neno la MUNGU kikawa na thamani kama chakula kidogo wakati wa njaa

MUHURI WA NNE (kanisa la Thiatira)

FARASI WA RANGI YA KIJIVUJIVU

 UFUNUO 6:7-8 Na alipoifungua muhuri ya nne, nikasikia sauti ya yule mwenye uhai wa nne akisema, Njoo! Nikaona, na tazama, farasi wa rangi ya kijivujivu, na yeye aliyempanda jina lake ni Mauti, na Kuzimu akafuatana naye. Nao wakapewa mamlaka juu ya robo ya nchi, waue kwa upanga na kwa njaa na kwa tauni na kwa hayawani wa nchi.

RANGI YA KIJIVUJIVU HUWAKILISHA NINI?-Rangi hii inaonyesha rangi ya mauti yenyewe.wanafunzi wa biblia  wameelewa kwa miaka mingi kuwa farasi wa nne  maana ya hali ya UFU YA KANISA la(zama za kati) wakati  kati ya mwaka 538 BK mpaka wakati matengenezo ya Kiprotestanti wakati ambapo kanisa liliokolewa sehemu tu kutoka nguvu  za UPAPA.

ROHO YA NCHI HUWAKILISHA NINI?-Robo ya nchi itakuwa basi na maana ya sehemu ya nchi ya mateso ya MAMILLIONI YA MASHAIDI WA WAKATI WA ZAMA ZA GIZA (538 BK-1517 BK)

MUHURI WA TANO.(kanisa la sardi)

UFUNUO 6:9-11 Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao. Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?  Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe, wakaambiwa wastarehe bado muda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile kama wao

NGUO NDEFU HUWAKILISHA NINI?-Kwa kawaida inaeleweka kwamba maneno NGUO NDEFU nyeupe huwakilisha heshima Kwa Mashahidi Waliokufa Kama KAFARA YA UPAPA.

MFANO WA WATU WALIOVIKWA NGUO NDEFU NYEUPE -Kwa maana ya kwanza watu Kama WYCLIFFE.HUSS NA JEROME walikuwa wamechukiwa na UPAPA walipewa heshima kuwa watumishi wa kweli wa Mungu. KIPINDI HIKI KILIANZA (1517-1798)

MUHURI WA SITA.(kanisa la Filadelfia)

UFUNUO 6:12-17 Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu, na nyota zikaanguka juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi. Mbingu zikaondolewa kama ukurasa ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake. Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,

MUHURI WA SITA ULIANZA (1798 A.D-1844 A.D)`Nyakati za zama za giza sasa zimekwisha pita na matukio makubwa yanaanza kutokea duniani .

KULITOKEA NA MATUKIO KAMA YAFUATAYO MOJA

TUKIO LA KWANZA LA TETEMEKO-Tetemeko kuu ambalo halijawahi kutokea mnamo asubuhi ya Novemba 1, 1755. karibu WATU 30,000 waliuawa katika muda wa DAKIKA SITA.

TUKIO LA PILI LA GIZA - -Tukio kubwa lilifuatia miaka michache baadaye siku ya Mei 19, 1780 siku ya kiza.

TUKIO LA TATU LA KUUNGUKA KWA NYOTA LILIFUATA-Nyota za mbinguni zikaanguka juu ya nchi Kama vile mti upukutishavyo mapooza yake Novemba 13.1833.

MUHURI YA SABA. ( kanisa la laodikia)

UFUNUO 8:1 Hata alipoifungua muhuri ya saba, kukawa kimya mbinguni kama muda wa nusu saa. Nami nikawaona wale malaika saba wasimamao mbele za Mungu, nao wakapewa baragumu saba.  Na malaika mwingine akaja akasimama mbele ya madhabahu, mwenye chetezo cha dhahabu, akapewa uvumba mwingi, ili autie pamoja na maombi ya watakatifu wote juu ya madhabahu ya dhahabu, iliyo mbele ya kiti cha enzi.

NINI KINACHOLETA KIMYA HIYO?-sura ya saba imetupwa kati  ya sura ya kufungua muhuri ya sita  tuliona waovu  wakiiambia miamba  na milima iwaangukie  na kuwasitiri mbele za uso  wake  yeye  aketiye juu ya kiti cha enzi na hasira  ya mwana kondoo

Mamia ya wengi wa wakaaji wa Dunia wameukataa msalaba na wamechagua kuangamia na hivyo wakati wakiangamia kuna kuwa kimya mbinguni

MUDA HUU WA NUSU SAA HUWALIKISHA NINI?- Nikipindi cha unabii ambacho siku ni sawa na mwaka mmoja basi kimya kitachukua kama juma moja.

No comments:

Post a Comment