Muda wa
majuma sabini umeamriwa juu ya watu
wako na juu ya mji wako mtakatifu ili kukomesha makosa ,na kushiliza dhambi ,na kufanya
upatanisho kwa ajiri ya uovu , na kuleta haki ya milele ,na kutia muhuri maono na unabii, na kumtia mafuta yeye aliye
mtakatifu . DANIELI 9:24-27
MALENGO
SITA YA MAJUMA SABINI
HUELEZEA
KIMSINGI KILE KITAKACHOKAMILISHWA NA MAISHA NA HUDUMA YA KRISTO HAPA DUNIANI.
1)
KUKOMESHA MAKOSA- HUMAANISHA
Makosa
kuhusu uvunjaji wa mahusiano baina ya Mungu na mwanadamu, Kwa njia ya kafara
yake pale msalabani. Yesu aliunganisha tena uhusiano uliokuwa umevunjika na
kutulejesha kwa Yesu
2)
KUISHIRIZA DHAMBI-HUMAANISHA
Gabriel
hapa anatangaza kuwa masihi
ataushugulikia udhaifu wa mwanadamu ,atazibeba dhambi
zao na hivyo kuziiishiliza( KUZIKOMESHA)
3)
KUFANYA UPATANISHO KWA AJIRI YA UOVU-HUMAANISHA
Uovu ni
dhambi kama ukiukaji walililosahihi kupitia kafara yake ya upatanisho pale
msalabani Yesu Kristo alishugulikia dhambi katika kila nyanja yake.
4) KULETA HAKI YA MILELE-HUMAANISHA
Kupitia
anguko wanadamu wamepotoka
na wasio haki
masihi aeleza Gabriel ataleta haki kutoka kwa Mungu ambayo itakuwa ni ya milele
kwa wote ambao huidai haki hii kuwa yao kwa njia ya imani iongozayo
katika utii.
5)
KUTIA MUHURI MAONO NA UNABII-HUMAANISHA
Wazo la
kutia muhuli hapa halikuhusu kufunga bali kuthibitisha kuidhinisha “ utimizo wa unabii kuhusu
kuwasili kwa msihii katika muda maalumu uliotajwa katika unabii huu
hutupatia uthibitivu kwamba mambo
mengine yaliyotabiliwa katika unabii
hasa hasa huo wa siku 2300 hakika utatimia
kama ilivyotabiliwa .
6)
KUMTIA MAFUTA YEYE ALIYE MTAKATIFU MNO -HUMAANISHA
Mahekalu
yalikuwa yanawekwa wakfu ili kuzindua
huduma zake( kutoka 40:9)
uwekwaji wakfu wa huduma ya Kikuhani ya kristo katika hekalu la mbinguni baada ya kupaa kwake WAEBRANIA 9:21
FAFANUZI
zaidi jina GABRIELI maana yake katika kiebrania
ni nguvu ya MUNGU au mtu wa MUNGU
Naomba
usikose masomo yanayofuata yanayohusu unabii huu wa majuma sabini somo linalofuata linasema NYAKATI MBILI
KUANZA PAMOJA
No comments:
Post a Comment