Monday, December 19, 2016

KWA NINI BAADHI YA WATU HUHISI KUNA MKONO WA MTU? WANAPOPITIA SHIDA TAABU NA MATESO?-S/N 4


MAANA YA MAJARIBU-Majaribu ni mvuto na ushawishi kufanya dhambi,nayo  hayatoki kwa Mungu ,bali kwa shetani  na kwenye  uovu wa moyoni mwetu sisi wenyewe.Mungu hawezi kujaribiwa na maovu,wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu. YAKOBO 1:13

JIFUNZE MAMBO TISA YANAYOELEZA UKWELI ULIVYO:

      I.            CHANZO KIKUBWA CHA MAJARIBU HUSABABISHWA NA TAMAA ZETU.

 Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu. Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.  Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti: YAKOBO 1:13-15

DHIKI KUU INAKUJA LAKINI KUNA TUMAINI SURA YA 17, UK, 141

Jaribu lenye  nguvu kushinda  yote halimpi mtu kisingizio chochote cha kutenda dhambi .haidhuru shinikizo linalowekwa juu  ya mtu  liwe kubwa kiasi gani ,uasi ni tendo  letu wenyewe.Haimo katika uwezo wa dunia wala wa jehanamu kumlazimisha mtu ye yote kutenda dhambi ,nia ya mtu ni lazima ikubali ,Moyo wake ni lazima  ukubali kutii ,ama sivyo tama ya mwili  haiwezi  kutawala  akili ,wala uovu kuishinda haki

   II.            KILA MMOJA ATAJARIBIWA   .                

  Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia. Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine. Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina HILO  1 PETRO 4:13-16,(1 Petro2:21,1:6-7,Waebrania 12:11 )

MLIMA WA BALAKA SURA YA 2, UK 47

(Heri wenye kuudhiwa kwa ajiri ya haki maana ufalme wa mbinguni ni wao)

Kama wanadamu wakijaribu  kupatana na Mungu wataona kwamba chuki ya msalaba  haijabadilika ,Falme na mamlaka  na majeshi ya pepo  wabaya  katika ulimwengu wa roho  hushindana  nao wote  wanaojitoa kuitii  sheria  itokayo juu ,kwa hiyo badala  ya kuhuzunika kwa sababu ya mateso ,INAWAPASA  WAFUASI WA KRISTO KUYAFURAHIA  MATESO ,kwani ndiyo  yanayoshuhudia ya kwamba wanazifuata nyao za Bwana wao.

III.            ILI UITWE MSHINDI UTAPITIA MAJARIBU MENGI.

Wakifanya imara roho za wanafunzi na kuwaonya wakae katika ile Imani, na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi MATENDO 14:22 :Wapenzi msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho. 1 PETRO 4:12

IV.            KUSTAHIMILI MAJARIBU

Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.  Yakobo 1:12, Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali; mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi. Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno:YAKOBO  1:2-4,

   V.            KUMBUKA  CHANGAMOTO UNAYOPITIA NI YA MUDA KITAMBO TU

Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.
Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana; tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.
     2 WAKORINTHO 4:16-18                 

MLIMA WA BALAKA SURA YA 2,UK 48

(Heri wenye kuudhiwa kwa ajiri ya haki maana ufalme wa mbinguni ni wao)

Kwa njia ya majaribu na mateso, tabia –YAANI SIFA YA MUNGU hufunuliwa kwa wateule wake . Watu kama kanisa la Mungu ambao huchukiwa na kuteswa  walimwengu huwa wakielimishwa na kuadilishwa  katika skuli ya kristo.hufuata njia nyembamba duniani;hutakaswa katika moto wa mateso.humfuta kristo katika mashindano makali  hustahimilin katika kujinyima   na kudhihakiwa lakini  katika maumivu ya mambo yanayowapata  watu wa Mungu  hujifunza  hatia na uovu wa dhambi jinsi ulivyo na jinsi unavyoleta huzuni ,nao huichukia sana dhambi  wakishiriki mateso ya kristo ndivyo watakavyokuwa washiriki wa utukufu wake.

VI.            MUNGU AMEANDAA MLANGO WA KUSHINDA CHANGAMOTO.

Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili  1 WAKORINTHO 10:13

VII.            ILI USHINDE JARIBU NI LAZIMA UWE NA IMANI              

Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye:   WAEBRANIA 10:38

MAANDIKO YA AWALI AU EARLY WRITING

SURA YA 8 UK 41: JARIBIO LA IMANI YETU

Katika wakati huu wa kujaribiwa  sisi  tunahitaji  kutiana moyo  na kufarijiana .majaribu ya sheteni  kwa sasa ni mengi zaidi kuliko ilivyowahihi kuwepo, maana anajua kwamba  muda wake ni mfupi  na kitambo kila kesi  itakuwa imeamuriwa aidha  kwa uzima au kifo .huu si wakati wa kuzama katika  hali ya kukata tamaa  na majaribu:tunapaswa  kuvumilia yote  yanayotuumiza  na kutumainia kabisa nguvu  zake Mungu  kabisa ,tunaweza kushinda  kila  jaribu  na kupata  ushindi kupitia neema yake.

SURA YA 8 UK 42: JARIBIO LA IMANI YETU

MUNGU amenionyesha kuwa yeye huwapa watu wake kukinywea kikombe kichungu ili kuwasafisha na kuwatakasa .ni kikombe kichungu ,lakini nao wanaweza kukifanya kiwe kichungu zaidi na zaidi  kwa kulalamika na kunungunika na kuona  uchungu.na wale wanaokipokea  kikombe hicho kwa malalamiko  na manunguniko inalazimika wapate kikombe  kingine maana kile cha kwanza  hakijafanya makusudi yake  moyoni .na kama kile cha pili hakitafaulu,atalazimika kupata kingine  na kingine .baada ya kingine mpaka makusudi ya Mungu  yafanyike  ama siyo  wataachwa kuwa wachafu na moyo usiotakaswa.niliona kuwa kikombe hiki  kichungu  kinaweza  kufanywa kuwa kitamu kwa  uvumilivu ustahimilivu na maombi.na  kwamba kitafanya makusudi yake kwa wale wote wanaokipokea kwa namna hiyo ,na Mungu ataheshimiwa na kutukuzwa.

VIII.            LENGO KUBWA LA  MAJARIBU NI KUKUTAKASA DHAMBI:

...... ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo  1 PETRO 1 :6-7

TUMAINI KUU, UK 324, SURA 32

(Kinasema namna ya kumshinda shetani/ushindi wa kutosha uk 325.)

BWANA anaruhusu watu wake wapate majaribu makali siyo kwa sababu anaifurahia dhiki yao lakini kwa ajili ya utukufu wake hawezi kuwakinga na majaribu kwani lengo la majaribu ni kuwatayarisha kwa ajili ya kuvipinga vivutio vyote vya uovu.

Watu waovu na mashetani  hawawezi kuuondoa uwepo wa Mungu katoka kwa watu wake endapo wataungana na kuziweka  mbali dhambi zao na kuzidai ahadi zake kila jaribu la wazi ama siri linaweza kupingwa  kwa mafanikio si kwa nguvu bali ni kwa roho yangu asema BWANA WA MAJESHI.

KITABU CHA PAMBANO KUU

SURA YA 30, UK 130 (shetani apigana na binadamu)

Kama tukiletwa katika majaribu tutakuwa na hakika kuwa Mungu atatulinda, lakini tukijipeleka wenyewe majaribuni tutaanguka tu bila shaka.

IX.            JE MUNGU ANAPENDA AU ANAFURAHI WATU WAKE WAPATE MATESO?

MAOMBOLEZO 3:33 Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha

MLIMA WA BALAKA SURA YA 2 UK 25-27

(Heri wenye huzuni maana hao watafarijika)

Hatupati mateso bila sababu ,kwani Mungu  moyo wake  hapendi kuwatesa  wanadamu ,Wala kuwahuzunisha.Mungu  anaporuhusu  tupatwe na majaribu na taabu ,Sababu yake ni kwa  faida  yetu ili  tuushiriki utukufu wake(WAEBRANIA 12;10) LILE JARIBU LINALODHANIWA KUWA NI UCHUNGU NA GUMU KULIVUMILIA ,LIKIPOKELEWA  KWA IMANI INAONEKANA KUWA NI MBARAKA ,Lile pigo kali  linalozimisha furaha  za Dunia  litakuwa njia  ya kuyageuza macho yetu  kuangalia juu  mbinguni .ni wengi ambao wasingelimjua YESU  isipokuwa  misiba  imewaongoza kutaka kufarijiwa naye

Taabu maishani  ni kama watenda kazi  wa Mungu  kwa kutoa uchafu  na mambo yaliyo maovu  katika tabia  zetu  na kutukamilisha  tuwe na sifa njema .katika kuchongwa  kukatwa  na kukwatuliwa  yapatikana maumivu –kukandamizwa kwa jiwe  la kunolea ,lakini Yule avumiliaye katika majaribu  mwishowe  atafanywa  kuwa kama jiwe zuri  la jingo la Mungu .Bwana hatendi kazi nyingi  kwa bidii hivi  kwa kitu  kisichofaa ili kwa vito vyake vya dhamani tu  vinavyonakishiwa vifae kwa jingo la hekalu

Lakini tukipatwa na shida ,wengi wetu hufanana  Yakobo.tunafikiri kuwa ni mkono  wa adui ulio juu yetu  nasi  tunashindana gizani hata nguvu zetu zimekwisha ,bila  bila kusaidiwa  wala kukombelewa ,yakobo alipoguswa  wakati  wa mapambazuko  akaona  kumbe  Yule aliyeshindana naye  ni malaika wa Mungu  naye Yakobo alipoona  hana  nguvu akajitupa mbele  yake apate mbaraka alioutamani kupata moyoni mwake ,Hata nasi pia inatubidi kujifunza kuwa majaribu yaweza kuwa  nafuu kwetu ,tusidharau kurudi kwake Bwana ,wala tusizimie moyo tukikemewa naye (WAEBRANIA 12:5)

 

ULIZA SWALI KAMA HAUJAELEWA

 

 

 

 

 

 

 

No comments:

Post a Comment