Monday, December 19, 2016

MASHARTI YA KUPOKEA MIBARAKA:-S/N 6


MAMBO MANNE TUNAYOJIFUNZA

      I.            ILI UPOKEE BARAKA AU UBARIKIWE NI LAZIMA UFANYE JAMBO MOJA TU  AMBALO NI KUTII 

TORATI 28:1

Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako,atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;

   II.            IFUATAYO NI ORODHA YA BARAKA KAMA MATOKEO YA UTII

TORATI 28:2-14

Na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako.Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani. Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng'ombe wako, na wadogo wa kondoo zako. Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga. Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo. Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako; ..................

III.            TAHADHALI UKIBARIKIWA USIFANYE JAMBO HILI

 TORATI 8:11-14,17 1

 Jihadhari, usije ukamsahau Bwana, Mungu wako, kwa kutozishika amri zake, na hukumu zake, na sheria zake, ninazokuamuru leo. Angalia, utakapokuwa umekula na kushiba, na kujenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake;  na makundi yako ya ng'ombe na kondoo yatakapoongezeka, na fedha yako na dhahabu yako itakapoongezeka, na kila kitu ulicho nacho kitakapoongezeka;basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau Bwana, Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa;

IV.            MUNGU HUTOA ADHABU KWA WALE WANAOTUMIA VIBAYA MIBARAKA YAKE.

MFANO MFALME NEBUKADREZA-kosa alilolifanya alijiinua na kujisifu aliadhibiwa kuwa mnyama na kula nyasi kwa miaka saba DANIELI 4:28-32   Hayo yote yakampata mfalme Nebukadreza. Baada ya miezi kumi na miwili, alikuwa akitembea ndani ya jumba la kifalme katika Babeli. Mfalme akanena, akasema, Mji huu sio Babeli mkubwa nilioujenga mimi, uwe kao langu la kifalme, kwa uwezo wa nguvu zangu, ili uwe utukufu wa enzi yangu?  Hata neno lile lilipokuwa katika kinywa cha mfalme, sauti ilikuja kutoka mbinguni, ikisema, Ee mfalme Nebukadreza, maneno haya unaambiwa wewe; Ufalme huu umeondoka kwako.  Nawe utafukuzwa mbali na wanadamu, ............  (,MITHALI 16:18)

MFANO MFALME HERODE-kosa alilolifanya hakumpa Mungu utukufu; MATENDO 12:20-23 Naye Herode alikuwa amewakasirikia sana watu wa Tiro na Sidoni; ....... Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi katika kiti cha enzi, akatoa hotuba mbele yao.  Watu wakapiga kelele, wakisema, Ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu. Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho.

MFANO MFALME SULEMANI-kosa alilolifanya alijitukuza na kutegemea hekima yake,kuabudu miungu,kuoa wake zaidi ya mmoja  Mungu alimwondolea ulinzi wake  na maadui zake wakaanza kumshambulia pande zote 1 WAFALME 11:14-28 Ndipo Bwana akamwondokeshea Sulemani adui, Hadadi Mwedomi; yeye alikuwa wa wazao wake mfalme wa Edomu.

USIPOTII MAAGIZO YA MUNGU BARAKA ZOTE ULIZOPEWA NA MUNGU ZINAGEUKA KUWA LAANA

 TORATI 28:15-29 Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata. Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani.  Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia.Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, ................

WITO ,YEREMIA 9:23-24:Bwana asema hivi, Mwenye hekima asijisifu kwa sababu ya hekima yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake; bali ajisifuye na ajisifu kwa sababu hii, ya kwamba ananifahamu mimi, na kunijua, ya kuwa mimi ni Bwana, nitendaye wema, na hukumu, na haki, katika nchi; maana mimi napendezwa na mambo hayo, asema Bwana


 

 

 

 

 

 

 

No comments:

Post a Comment